College History


THE HISTORY OF TANDALA TEACHER COLLEGE


Chuo cha Ualimu Tandala kilianzishwa mwaka 1975 na kiko katika Wilaya ya Makete Mkoa wa Njombe. Chuo kipo umbali wa kilometa 85 kutoka makao makuu   ya Mkoa na kilometa 30 kutoka makao makuu ya Wilaya. Chuo hiki kilianzishwa kwa madhumuni ya kutekeleza Agizo la Musoma lililohusu kufikiwa kwa Elimu kwa Wote (UPE) ifikapo mwaka 1977. Chuo kilirithi majengo ya iliyokuwa Shule ya Kati (Middle School) iliyokuwa ilimilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kusini Kati, kutokana na mahitaji ya walimu yaliyosababishwa na ongezeko la wanafunzi wa shule ya msingi kanisa kwa hiari yake lillitoa majengo ya shule hiyo kwa lengo la kuanzisha mafunzo ya Ualimu.

Mafunzo ya Ualimu ambayo yamekuwa yakitolewa tangu Chuo kilipoanza ni pamoja na Daraja la IIIC (1975 – 1985), Daraja la IIIB (1985 – 1996), Daraja la IIIA (1994 – 2015), mafunzo ya Walimu kazini kuanzia daraja la CB hadi A (MUKA) kuanzia 2004 hadi 2007. Kwa sasa Chuo kinaendesha Programu mpya ya Mafunzo ya Walimu kwa Ngazi ya Diploma.


NEW:MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2015 BOFYA HAPA

0 comments:

Post a Comment

Note: only a member of this blog may post a comment.